Wananchi pwani ya Kenya washinda kesi dhidi ya mchafuzi wa mazingira

Get monthly
e-newsletter

Wananchi pwani ya Kenya washinda kesi dhidi ya mchafuzi wa mazingira

Wakazi 3,000 walioathiriwa na sumu ya madini ya risasi wapewa fidia ya dola milioni 12, ingawa usafi bado haujafanywa.
Christabel Ligami
Afrika Upya: 
21 December 2020
Bi Phyllis Omido kushoto, mmoja wa wahasiriwa wanaoongoza kwa sumu, na wakili wake katika korti ya..
Christabel Ligami
Bi Phyllis Omido kushoto, mmoja wa wahasiriwa wanaoongoza kwa sumu, na wakili wake katika korti ya sheria ya Mombasa baada ya kushinda kesi hiyo.
Ikiwa huwezi kusoma sasa, sikiliza tu toleo la sauti: 
Sauti hii iko kwa Kiingereza.

Ilisifiwa nchini kama moja ya kampeni kubwa zaidi katika muongo huu, mnamo mwaka 2016, mtaalam wa mazingira wa Kenya Phyllis Omido alianza vita dhidi ya sumu ya madini ya risasi na betri ya asidi iliyokuwa ikiyeyushwa katika makazi duni ya Owino Uhuru, katika mji wa pwani ya Mombasa.

Bi. Omido, 42, alienda mahakamani kwa niaba ya wakazi 3,000 wa eneo hili, na miaka minne baadaye, mnamo 16 Julai 2020, mahakama iliamua upande wao, ikitoa fidia ya dola milioni 12 kwa wale walioathiriwa na sumu ya madini ya risasi.

Pesa hizo zilikuwa zitumike kwa matibabu yao na fidia ya vifo vilivyotokana na sumu hiyo.

Serikali ilikuwa ilipe ndani ya siku 90 kwa kushindwa kutekeleza kanuni za mazingira na kuichukulia hatua kampuni hiyo ya Metal Refinery EPZ, ilipofunguliwa kwa biashara mnamo mwaka 2007 na kufungwa mwaka 2014.

Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa  serikali  na Mamlaka ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mazingira (NEMA) waliwasilisha rufaa dhidi ya uamuzi huo.

Katika ombi la kukata rufaa, NEMA ilisema kuwa bajeti yao haikuwa kubwa ya kutosha kulipia usafishaji wa makazi hayo, huku ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ikisema haijaridhika na uamuzi huo kwa kuwa dhima ya fidia, kusafisha na matibabu ya wakazi yanapaswa kuchukuliwa na kampuni ya kuyeyusha chuma na si serikali.

Lakini Bi. Omido hajachoka, amezindua kampeni dhidi ya rufaa ya serikali. Kupitia shirika lake, Kituo cha Haki, Utawala na Mazingira (CJGEA), mkakati huo pia unatarajiwa kutafuta fedha za dawa na matibabu kwa wale wanaopata athari ya sumu ya  madini ya risasi.

"Tunaposubiri rufaa, tuna waathirika waliolazwa hospitalini, wale wanaoishi na magonjwa ya figo na ini kushindwa kufanya kazi na watoto wengi walio na magonjwa ya ngozi. Yote haya ni matokeo ya sumu ya madini ya risasi, ”alisema Bi Omido.

Bi. Omido anasema kuwa hadi sasa kampeni hiyo imekusanya dola 1,000. Uamuzi wa rufaa ya serikali unatarajiwa kutolewa tarehe 17 Februari 2021.

 “Hakuna chochote kinachoweza kufanyika kwa sababu ya ombi la kukata rufaa la NEMA na ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali. Kila kitu ikiwemo kusafisha makazi, matibabu ya wagonjwa — kitalazimika kusubiri hadi uamuzi wa rufaa utolewe, ”alisema Bi. Omido.

Bi. Omido, ambaye aliongoza kampeni ya kufunga kiwanda cha kuyeyusha chuma mnamo mwaka 2014, alifanya kazi kupitia CJGEA kuwasilisha kesi hiyo mahakamani mnamo mwaka 2016, akitaka fidia na haki kwa wale walioathiriwa na sumu ya madini ya risasi katika eneo la Owino Uhuru baada ya majaribio kadhaa ya kuzungumza ili kukubaliana na serikali na taasisi nyingine husika kushindikana.

Katika uamuzi wake wa mwaka 2020 Jaji Anne Omollo aliona kuwa haki za jamii ya Owino Uhuru ya mazingira yenye afya, maji safi na salama, na maisha zimekiukwa na hivyo serikali na kiwanda cha kuyeyusha chuma kinapaswa kulipa fidia hiyo.

Ms. Omido the environmental activist and chief campaigner for the Owino Uhuru slum lead poison victims.
Bi Omido mwanaharakati wa mazingira na mwanaharakati mkuu wa kitongoji duni cha Owino Uhuru aongoza waathiriwa wa sumu. Picha: Christabel Ligami

NEMA, taasisi ya serikali inayohusika na mazingira, na kampuni ya kuyeyusha chuma waliamriwa kusafisha eneo hilo — udongo, maji na taka —kwa ajili ya masalia yoyote ya sumu ya madini ya risasi. Kukosa kufanya hivyo kungesababisha faini ya dola milioni 7 kwa CJGEA kuandaa na kuratibu usafishaji huo.

Mnamo mwaka 2015, Kamati ya Seneti ya Kenya pia ilifanya "utafiti" kuhusu sumu ya madini ya risasi kwenye eneo hilo na kugundua kuwa kweli kulikuwa na dalili za sumu ya madini ya risasi katika mazingira na kwamba watoto walionyesha dalili za kuathiriwa na  sumu ya madini ya risasi katika vipimo vya damu.

Kisha Seneti ilihitimisha kuwa mazingira hayo hayakufaa kwa maisha ya binadamu na ilipendekeza kwamba serikali ishughulikie sumu hiyo na kufanya usafi wa eneo hilo.

"Tulipogundua kuwa mashirika ya serikali hayana ujuzi juu ya kusafisha mazingira ya sumu ya madini ya risasi, tulileta wataalam kutoka Marekani kufundisha mashirika ya serikali jinsi ya kusafisha sumu ya madini ya risasi katika mazingira," Bi. Omido alisema.

ILi Fung, Mshauri Mwandamizi wa Haki za Binadamu katika Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa (OHCHR) anasema hukumu ya kihistoria ya mwaka 2020 ya mahakama ilikuwa ni ushindi kwa jamii, watetezi wa haki za binadamu za mazingira kama Bi. Omido, na kwa haki ya mazingira kwa ujumla. 

"OHCHR inaendelea kumsaidia Phyllis [Bi. Omido] na shirika lake,” anasema Bi. Fung. "Ni muhimu tuchukue hatua kudumisha na kutetea nafasi ya raia kwa watetezi hawa wa haki za binadamu kuendelea na kazi yao muhimu."

Mada: