Huku shule zikiwa zimefungwa, kuna mwanga wa matumaini katika mafunzo ya usimbaji wa kompyuta

Get monthly
e-newsletter

Huku shule zikiwa zimefungwa, kuna mwanga wa matumaini katika mafunzo ya usimbaji wa kompyuta

Mwarumba Mwavita
Afrika Upya: 
28 January 2021
Kambi ya boot ya siku 10 ya wasichana wadogo kutoka Afrika kote.
UNECA
Kambi ya boot ya siku 10 ya wasichana wadogo kutoka Afrika kote.
Ikiwa huwezi kusoma sasa, sikiliza tu toleo la sauti: 
Sauti hii iko kwa Kiingereza.

Mara nyingi, hadithi hujitokeza katika mzunguko wa habari kuhusu COVID-19 inayotoa mwanga wa matumaini katika bahari ya takwimu inayofisha moyo kuhusu watu kulazwa hospitalini pamoja na vifo.  Mwanzoni mwa mwezi Desemba 2020, mafunzo ya siku 10 ya usimbaji wa kompyuta kwa zaidi ya wasichana wadogo 2,000 kutoka barani Afrika, yaliandaliwa na Tume ya Kiuchumi ya Umoja wa Mataifa ya Afrika na Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ya Simu, jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Wasichana hao, waliotoka katika mazingira mbalimbali ya kiuchumi-jamii, walijifunza kutengeneza programu za kompyuta, Masuala ya Tovuti, Ufumaji wa Kasa (Turtle Stitch), AI, uundaji wa wavuti na elimu muhimu kuhusu haki za binadamu pamoja na ujasiriamali miongoni mwa taaluma nyinginezo. Mafunzo mengi yaliendeshwa mtandaoni.

Wakufunzi hao kutoka nchi mbalimbali barani Afrika, waliwapa changamoto wasichana hao kutengeneza Programu ili kutatua matatizo ambayo aidha wamekuwa wakikumbana nayo au kushuhudia wakati wa janga kubwa la COVID-19. Matokeo yalikuwa ni ya aina yake, sio tu katika kiwango cha kiufundi, bali pia ujuzi wa wasichana hao katika kushirikiana na kufanya kazi kama timu, misingi ya kiujasiriamali, kuimarisha viwango vya ujasiri katika mawasiliano ya kuongea pamoja na maandishi.

Kama mkuu wa zamani wa shule-aliyegeuka kuwa msomi, katika taaluma yangu yote nimejikita katika elimu na mapungufu yake. Lakini kwa wakati wote haijawahi kutokea changamoto ya ufikiaji kwa usawa wa shule kuwa ni suala la dharura kama wakati huu wa janga kubwa la COVID-19.

Kwa miongo mingi kabla ya COVID-19, wana elimu pamoja na watunga sera barani Afrika walikabiliana na masuala kadhaa na chaguzi kuhusu kujenga shule - shule mpya, usawa; kuimarisha ufikiaji kwa wasichana, watu walio pembezoni, walio kwenye mazingira hatarishi na kwa ujumla wale walio na uhitaji na majaribio na kompyuta-mpakato mashuleni.

A 10-day coding boot camp for over 2,000 young girls from around Africa
Wasichana wadogo kutoka kote Afrika kwenye kambi ya siku 10 ya kuweka alama. Picha: UNECA

Hata pale ambapo ufikiaji unawezekana, suala la ubora wa elimu limekuwepo, umuhimu wa mtalaa na kuhakikisha kwamba ujuzi na maarifa yanayofundishwa shuleni yanaambatana na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira. Kwa mantiki hii, baadhi wametoa hoja ya kusikitisha kwamba masomo ya STEM ni muhimu kuliko masomo ya ubinadamu - hata kudhihaki umuhimu wa michezo, sanaa na ubunifu.

Mtoto wa kike

Kwa mtoto wa kike katika nchi nyingi za Afrika, ufikiaji wa elimu haujawahi kuwa ni jambo ambalo amehakikishiwa. Lakini kwa kupitia mifumo kama vile Jukwaa la Beijing Platform for Action, hatua maridhawa zimepigwa. Ilhali, kuna mazungumzo mengi siku hizi ambayo hayajaangaziwa kwenye kutokuwepo mbioni kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu ya 2030 (SDG).

Wakati kuna vipaumbele vingi, huenda nchi za Afrika zikaendelea kuhangaika ili “kuhakikisha elimu bora na jumuishi na kuhamasisha fursa za muda mrefu za kujifunza kwa wote” kufikia 2030 (SDG 4) kwa muda mrefu ujao – kwa wasichana pamoja na wavulana na si vigumu kuona ni kwa nini.

Wakati COVID-19 ikiendelea kuathiri watu ulimwenguni kote, makadirio ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ya hasara za mafunzo yanaashiria kwamba asilimia 25 ya wanafunzi huenda wasitimize kiwango cha kimsingi kinachohitajika kushiriki kwa ufanisi na kuongeza tija katika jamii na katika fursa za baadaye za kujifunza.

A 10-day coding boot camp for over 2,000 young girls from around Africa
Kambi ya boot ya siku 10 kwa wasichana zaidi ya 2,000 kutoka Afrika. Picha: UNECA

Ulimwenguni kote, watoto milioni 23.8, vijana wadogo na vijana kutoka kiwango cha chekechea hadi elimu ya juu huenda wakaingia katika mwaka mpya bila  kitu chochote cha kujivunia. Huenda wengine wakawa wameacha masomo au hawana uwezo wa kufika shuleni kutokana na athari ya kiuchumi tu kutokana na janga hili kubwa, ikiwa ni pamoja na wasichana milioni 11.2 na wanawake wadogo.

Ripoti ya UNESCO inasikitisha na kukadiria kwamba hadi wasichana milioni 20 na wanawake wadogo katika nchi za uchumi wa chini na wa kati hawatarudi shuleni ulimwenguni kote. 

Barani Afrika, hali hii ni mbaya zaidi, kama ilivyoripotiwa katika ripoti ya UNESCO ya mwaka 2020 ya Elimu kuhusu Mapambano dhidi ya COVID-19, asilimia ya juu zaidi ya wasichana katika viwango vyote vya elimu huenda wakaathirika (1.99%), ikilinganishwa na wavulana (1.90%). Isitoshe, elimu ya chekechea itaathirika vibaya huku usajili ukitarajiwa kupungua kwa asilimia 7.9 kwa wasichana na wavulana. Wanafunzi wanaoishi katika umaskini na walio pembezoni na wale walioathirika wa mizozo na uhamaji ndio wataathirika zaidi. Suala hili linafaa kumpa wasiwasi mtunga sera yeyote. Hakika, ni ukweli unaotisha wa kupambana na madhara ya kiuchumi ya janga kubwa la COVID-19, au wale wanaolazimika kufanya maamuzi yanayodidimiza mustakabali wa watoto wao.

Masomo ya Usimbaji ya Kompyuta

Na hapa ndipo hadithi ya masomo ya kompyuta inatia moyo. Mpango huu ni mfano wa jinsi taasisi zinavyoweza kufanya ili kuongeza uwezo wa kufikia mafunzo wakati shule haziwezi kufikiwa. Kusomea kompyuta kunawezesha. Kunatoa mwanga wa matumaini na kufungua uwezekano kwa wasichana wadogo kukabiliana na changamoto ambazo haziongelewi, ikiwa ni pamoja na kubeba mizigo ya kaya, msongo wa mawazo, masuala ya afya ya akili na unyanyasaji katika mazingira ya COVID-19.

Kwa mtoto wa kike katika nchi nyingi za Kiafrika, upatikanaji wa elimu haukuwahi kuhakikishiwa kila wakati. Lakini kupitia mifumo kama Jukwaa la Utekelezaji la Beijing, hatua za kawaida zimepatikana.

Kutoa elimu bora na sawa kwa wote ni changamoto kubwa wakati huu. Kujiimarisha vyema baada ya wakati mgumu kutahitaji ubunifu mkubwa ili kufikia mkondo wa fursa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na sayansi endelevu, teknolojia, uhandisi na hisabati ili kuleta ari kwa Afrika kuwa bara la viwanda. Masomo ya kompyuta yanatoa mwanga wa matumaini wa kile kinachowezekana wakati juhudi zinafanywa kutengeneza fursa kwa wasichana na wanawake wadogo.

Nikitazamia 2021, nina matamanio mawili:

Kwanza, ningependa kuona taasisi nyingi zaidi zikijiunga na kushirikiana na shule za mitaa na jamii barani Afrika kuunda fursa za masomo ya kompyuta ya viwango vidogo kwa wanafunzi ambao wanauhitaji. Kampuni za mawasiliano zinaweza kutoa vipimo data bila malipo ili kufanya masomo ya kompyuta kuwezekana na kusaidia mbinu za kiubunifu za masomo ili kuzuia wanafunzi kuacha shule na kusababisha hasara za mafunzo.

Pili, ningependa kuona harakati ambapo watu binafsi wanaleta matumaini kwa wanafunzi ambao wanalazimika kuacha shule. Kuanzia kuchanga karo za shule hadi kuwa washauri na kuchukua nafasi kama vielelezo, sote kama watu binafsi katika jamii zetu, tunaweza kusaidia vijana na watoto kujihusisha na kujifunza na katika elimu rasmi. Pamoja na sera endelevu za serikali, harakati inayochukua hatua katika ngazi ya chini inapaswa kuondoa takwimu za UNESCO kwa asilimia moja baada nyingine.


Dkt. Mwarumba Mwavita ni  Mkurungenzi Mwanzilishi wa Kituo cha Utafiti na Tathmini za Elimu na Profesa Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Oklahoma State ambapo anafundisha tathmini, ukadiriaji na takwimu. Anafanyia utafiti STEM, sera ya kielimu, uwajibikaji, tathmini ya sera, mbinu za viwango anuwai na uchanganuzi wa takwimu kilongitudo. Nchini Kenya, yeye ni mhadhiri katika Vyuo Vikuu vya Strathmore na Moi. Twitter: @MwarumbaM

 

 

Mwarumba Mwavita
More from this author