Kupambana na ‘janga la kinyumbani’: Umoja wa Afrika unapongeza Chapisho la Sauti Blog kwa kujihusisha na vita dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia

Get monthly
e-newsletter

Kupambana na ‘janga la kinyumbani’: Umoja wa Afrika unapongeza Chapisho la Sauti Blog kwa kujihusisha na vita dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia

Mwandishi mchanga wa kike anahamasisha ufahamu kuhusu mivutano iliyopo baina ya kuhifadhi taswira ya umma na kunusurika unyanyasaji wa kinyumbani.
Franck Kuwonu
Afrika Upya: 
28 September 2020
Ukatili wa kijinsia
UNFPA
Wakati nchi nyingi zinaripoti kuambukizwa na kufungwa, nambari zaidi za msaada wa unyanyasaji wa nyumbani na makao kote ulimwenguni zinaripoti kuongezeka kwa wito wa msaada.

"Mke wa anayejitolea lakini ambaye amekabiliwa na 'janga la faragha'”, Debbie anasita kupokea msaada uliotolewa na Mama Mary ambaye, alipokutana naye kwa mara ya kwanza, alitambua ishara za mke anayepigwa akiwa katika ndoa ya dhuluma.

Ruth Nyadzua Mwangome
Ruth Nyadzua Mwangome

Mama Mary, Debbie na Mchungaji Karisa (mumewe Debbie) ndio wahusika watatu katika The Domestic Pandemic (Janga la Kinyumbani) hadithi fupi iliyoandikwa na Ruth Nyadzua Mwangome, mwandishi kijana kutoka Kenya.

Bi. Mwangome ni mmoja kati ya watu ambao kazi zao zimechapishwa katika blogi ya Sauti صويت, mkusanyiko wa kidijitali wa hadithi 25 za wanawake vijana kutoka Afrika kuhusu athari za COVID-19.

Chapisho hili, lililozinduliwa na Ofisi ya Umoja wa Afrika ya Mjumbe wa Vijana, linalenga kupongeza wanawake vijana wa Afrika walioko katika mstari wa mbele kupambana na COVID-19 na kuonesha talanta zao za kibunifu.

Katika mahojiano haya mafupi na Afrika Upya, Ruth Nyadzua Mwangome anazungumzia hadithi yake inayohusu unyanyasaji wa kinyumbani wakati wa COVID-19: Hapa chini ni madondoo:

Je, Sauti صويت blog ni nini?

Ni mkusanyiko wa msururu wa hadithi 25 za wanawake vijana wa Kiafrika kuhusu athari za #COVID19. Ni jukwaa la kuinua na kusherehekea uthabiti na uvumbuzi wa wanawake vijana wa Kiafrika katika "kawaida mpya" na kutetea zaidi masuala yanayowaathiri kila siku, kulingana na Bi Aya Chebbi, Mjumbe wa Vijana wa Umoja wa Afrika.

Sauti صويت blog ni nafasi mbadala inayobeba maadili ya kifeministi ya Umoja wa Afrika na inabadilisha mtazamo kwa sababu mapambano yetu kama wanawake vijana wa Afrika ni mapambano ya kusikika,” asema Bi. Chebbi.

Afrika Upya: Tufahamisha kuhusu wahusika katika hadithi yako?

Ruth Nyadzua Mwangome: Mchungaji Karisa, mkewe Debbie na Mama Mary wote ni waumini katika kanisa moja, lakini wanakabiliwa na mashetani binafsi ambayo yanaongezeka wakati janga la COVID-19 linazuka.

Debbie ni mke wa kujitolea ambaye amekabiliwa na 'janga la kibinafsi' (unyanyasaji wa kijinsia - GBV) na COVID-19 imekuja kama janga la pili. Maisha yake yako hatarini lakini anasita kupokea msaada kwa sababu ya kile jamii inatarajia kutoka kwake. Yuko katika uongozi na anaona haja ya kulinda taswira hiyo ya 'umma.' Ana wasiwasi kuhusu kumwacha mumewe na kudhaniwa na jamii kuwa alishindwa kudumisha ndoa.

Kwa upande mwingine, mumewe Mchungaji Karisa, anafaa kuwa mfano wa kuigwa. Lakini kushindwa kwake kumefunuliwa na kutokuwa na uhakika na mapungufu yaliyoletwa na COVID-19.

Mwishowe, Mama Mary ni manusura ya unyanyasaji wa kijinsia na mwanaharakati. Anasikitishwa na dhuluma wanayofanyiwa wanawake. Lakini kwa macho ya madume, yeye ni "mwanamke mwendawazimu." Dalili zinazoonekana za unyanyasaji zinamfanya ajaribu kumkomboa Debbie kutoka kwa mtego wa unyanyasaji wa kinyumbani.

Kwa nini unawalete wahusika hawa pamoja kwa njia hii katika hadithi?

Masuala ya imani ni nyeti sana na mara nyingi huachwa bila kuguswa. Licha ya hayo, kuna watu walio katika imani wanaoteseka kimyakimya na wanahitaji msaada. Wengi wao wanakataa au hata wanaogopa kusema. Kusimulia hadithi kama hii kunasaidia kuwaelimisha wao na wengine kuwa mambo kama hayo hutokea lakini kilicho muhimu ni kwamba kuna msaada. Kile mtu anahitaji kufanya ni kupaza 'sauti' yake.

Je, hii in bunilizi tu au ni hadithi ya kweli? 

Ni mchanganyiko wa matukio ya kweli na ya kubuni. Kuiandika kama insha kungezuia mawanda mapana niliyokusudia iwe nayo. Majina ni ya kubuni, lakini hali ni ya kweli katikati ya janga la COVID-19. Kwa bahati mbaya, jukumu la Mama Mary ambalo ni muhimu sana, ni la kubuni.

Je, kuna ujumbe maalum unaojaribu kuwasilisha?

Ndiyo. Kwanza, mtu yeyote anaweza kuwa mwathiriwa wa unyanyasaji wa kinyumbani na wala haijalishi hadhi yake katika jamii na pia kuwa mnyanyasaji anaweza kuwa wa aina yoyote.

Pili, tamati ya hadithi haionyeshi kile ambacho hutokea katika maisha halisi. Nilichagua kuandika hadithi jinsi nilivyofanya ili kupendekeza suluhisho au chaguo kwa yeyote aliye katika wadhifa wa uongozi ambaye bado anakabiliwa na hali kama hiyo.

Tatu, wanawake ni walinzi wa kila mmoja, kwa hivyo wanakuwa waangalifu kwa dalili za unyanyasaji wa kijinsia na kuwasaidia akina mama, dada, shangazi au binti anayehitaji msaada. Tunahitaji watu wengi kama Mama Mary katika jamii.

Wewe ni miongoni mwa washindi 25 wa shindano la Sauti Blog. Je, uliandika hadithi hiyo kwa mashindano tu au hii ni hadithi iliyolenga suala hili?

Nilikuwa na hadithi hii, lakini sikuweza kupata fursa ya kuiandika. Kwa hivyo, mashindano ya Sauti Blog ilikuwa fursa ya kipekee. Nilipopata fursa hii, nilifurahi na kunyenyekea kwani nilijua kuwa hapo, ingehamsisha hadhira kubwa.

Bonyeza hapa ili usome Domestic Pandemic na  hapa kusoma msururu wote wa Sauti صويت blog